NA.GOODLUCK CHRISTOPHER.
Wananchi wa Katubuka manispaa ya kigoma ujiji wameilalamikia
serikali kufuatia kufutika kwa alama za kivuko vya watembea kwa miguu katika
barabara ya uwanja wa ndege hali inayo pelekea kutokea kwa ajari pindi wanapo vuka barabara.
Maurid Ally ni mmoja kati ya wakazi wa mwanga ambae amesema
kuwa kufutika kwa vivuko hivyo ina sababisha kutokea kwa ajari kutokana na
madereva wa vyombo vya moto kama Magari,Bajaji na Pikipiki kupita kwa kasi
pasipo kuzingatia uwepo wa alama hizo.
Aidha Ally amesema kwamba katika mwaka uliopita
alishuhudia mtoto mmoja akigongwa na gari huku wengine wakijeruhiiwa mara kwa
mara hususa ni wanafunzi washule ya msingi ya Katubuka pamoja na Mwenge.
Kwa upande wake Ashel Kaguta ambae pia ni mkazi wa
eneo hilo amesema kuwa hili ni tatizo kubwa hususa ni nyakati za usiku ambapo
madereva hutembea kasi huku wengine wakiwa ni wageni wa njia hiyo.
Vilevile Kaguta amemaliza kwa kusema kuwa serikali
wanapaswa kuliangalia tatizo hili kwa jicho lapili ili kunusuru wakazi waeneo
hilo hususa ni watoto washule.
Sikuishia hapo nikaumua kumtafuta meneja wa TARURA Manispaa ya kigoma ujiji Bw. Issa Ally Ryanga
ambae amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na kuahidi kuwa wanapanga bajeti kwa ajiri
ya kuweka alama hizo haraka iwezekanavyo.
Pia Ryanga amemaliza kwa kusema kuwa si kufutika kwa
alama hizo tu bali wanatarajia kufukia mashimo pamoja na kurudishia alama zote
za barabarani [road singn] kwasababu havihitaji pesa nyingi kurekebisha.
Ikumbukwe kuwa barabara hii ni moja kati ya barabara
ambazo zimefutika alama hizo katika manispaa ya kigoma ujiji yingine ikiwa ni
barabara ya Noradi ,Kibirizi n.k


0 Maoni