Mwafrika Digital

https://youtu.be/ArXfq-5TVWA Subscribe Mwafrika TV

VYOO VYA HATARISHA MAISHA YA WATU KIGOMA UJIJI

NA.GOODLUCK CHRISTOPHER
Ni takribani mwezi mmoja tangu vyoo vya kituo cha daladala cha ujiji katika manispaa ya kigoma ujiji kujaa na kutelekezwa jambo linalo hatarisha maisha ya madereva pamoja na abiria wanao tumia kituo hicho.
TUNAOMBA RADHI KWA MUONEKANO WA PICHA HII HAPO JUU.

Plan Media ilipata kufika katika kituo hicho kujionea haliharisi pamoja na kuzungumza na baadhi ya madereva lakini pia abiria ambao wameitupia lawama chama cha wamiliki wa Daladala mkoa wa Kigoma KIBOA kwa kushindwa kurekebisha miundombinu ya vyoo hivyo.

Aidha Samwel Gabliel ni mmoja wa madereva ambae amesema kuwa wamekua wakilipia shilingi 1000 kwa kila siku lakini wakiingia katika vyo hivyo wanashindwa kujisaidia kutokana na kujaa pasipo kufanyiwa usafi.

Kwa upande wake Mrisho Mashaka amesema kuwa imefikia hatua wanalazimika kutumia vyoo vya nyumba zinazo patikana karibu na  kituo hicho jambo ambalo ni usumbufu kwao ikilinganishwa na kipidi hiki cha masika ambapo ni rahisi kupatwa na magonjwa ya mlipuko.

Vilevile Addul Juma ni mmoja wa abiria anae toka Ujiji kuelekea Kibirizi kuwa haoni haja ya kupandia gari ndani ya kituo hicho kwasababu kituo hicho hakina manufaa kwa watumiaji na badala yake anaamua kusubiria gari nje ya kituo hicho.

Hata hivyo watumiaji wa kituo hicho wameuomba uongozi wa wamiliki wa daladala kwa mkoa wa Kigoma KIBOA kurekebisha miundo mbinu ya vyoo hivyo ili kuwanusuru na afya zao kutokana na magonjwa ya mripuko yanayo weza kujitokeza.

Plan Media haikuishia hapo ikaamua kumtafuta Mwenyekiti wa KIBOA  BW. Ibrahim Zubari ili kujua mwafaka wa tatizo hili ambae ameonesha kuto kujua tatizo hili na kuahidi kwamba analifanyia mchakato ili liweze kutatuliwa.

Vilevile Zuberi amekana kupokea kiasi cha Sh.1000 na kufafanua kuwa pesa hiyo ni tozo ya manispaa ambayo madereva hao wanapaswa kutozwa katika vituo vyote vya daladala ndani ya manispaa ya kigoma ujiji.


Ikumbukwe kuwa mkoa wa kigoma ni moja kati ya mikoa ambao umekua ukikumbwa na ugonjwa wa kipindupindu hususa ni ukanda wa ziwa Tanganyika na chanzo ikiwa ni baadhi ya watu wasio na utu kujisaidia pembezoni mwa ziwa hilo, hivyo basi hatua zinapaswa kuchukuliwa haraka iwezekanavyo ili kujiepusha na madhara makubwa yanayo weza kujitokeza katika kituo hicho.

Chapisha Maoni

0 Maoni