CCM yabomoa ngome ya
CUF, Kumbilamoto asema bado Picha kamili. KAMPENI za Udiwani zimeendelea Leo
Kata ya Vingunguti, huku tukishuhudia Ngome ya CUF ikizidi kumeguka vipande
vipande hii ni Mara baada ya Viongoz wa juu kurudisha kadi zao na kujiunga CCM.
Akizungumza katika
Kampeni hizo, Julius Mtatiro, amesema kwamba chama cha CUF inatafunika vipande
vipande kwa ajili ya ubinafsi wa vyama vya upinzani huku kikikosa muelekeo.
Amesema kuwa wato hao wamejiunga na CCM
kumfuata Kumbilamoto kutokana na madudu yanayofanywa na chama hicho .
Pia amesema kuwa ,
mwaka 2011, CUF kilifanikiwa kuwa na wabunge 2 kwa Tanzania bara na
zaidi ya madiwani 200.
Hata hivyo amesema
mwaka 2015 CUF ilipata jumla ya madiwani 400 na kufanikiwa kuongoza
Halmashauri ambapo ni mabadiliko makubwa ndani ya chama hicho kilichokuwa kina
wasomi wachache na kupambana kupata wasomi.


Amesema Vyama vya
upinzani havina malengo ya muda mrefu kwani akili zao zimeegemea na
kulenga kupata wabunge na madiwani bila ya kuwa na mipango ya kisiasa.
Hivyo amesema Madiwani wengi na wabunge wa CUF
watajiondoa huko kutokana na sarakasi zinazoendelea na ukosefu wa muelekeo wa
kisiasa.
Wakati huo huo akieleza mustakabadhi wa
vijana, amesema Vijana wengi wanaingia katika majukwaa ya kisiasa kwa ajili ya
kutafuta fursa za kutumikia kwa vipawa vyao katika kutafuta mbinu mbadala za
kutatua kero na kupambana na umasikini. " Lazima niwe mkweli, nchi hii
ikifikia wakati watu wenye Pesa hawashikiki , Leo Rsis Magufuli
amewatuliza na amerejesha Heshima ya Taifa hili LA masikini na Wanyonge Sasa
utashindwaje kuunga mkono? Halafu upinzani tunapinga "amesema Mtatiro.
Serikali ya awamu ya
tano tangia iingie madarakani kuna Mabadiliko makubwa sana ya kimaendeleo,
hivyo ili ufanye kazi vizuri na kuitendea haki nafasi yako Hamis CCM utakuwa
huru .
Naye Omary
Kumbilamoto, amesema yeye siye mzungumzaji sana Bali yupo katika
kusimamia Yale anayoyaahidi kwa vitendo. Hivyo amewaomba wana Vingunguti
wasifanye makosa wazidi kumuamini ili azidi kuwatimizia Yale wananchi
wanayoyataka na kuyaahidi katika utatuzi wa kero. "Ndugu zangu nataka
kuwaambia hii Picha iliyojitokeza Leo ni kisanga kikubwa bado mafuriko yanakuja
hivyo wale mliobakia CUF rudini nyumbani kumenoga" amesema Kumbilamoto.
Mbali na Kumbilamoto,
aliyekuwa Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Mtakuja, Ndugu Sharif Mbulu,
amesema kuhama kwake chama kumetokana na mgogoro unaoendelea CUF , hivyo
ameipongeza Kamati kuu ya CCM kwa kumpokea vizuri na yupo tayari
kushirikiana nao.
"Nimeachia nyadhifa zangu zote zikiwemo za Serikali na kujiunga CCM, Mimi sio mjinga nimepima kina cha Maji nikaona siwezi kuyavamia na nimeungana na Ndugu yangu Kumbilamoto kwani ameniachia majukumu mwezi sasa sitoki nje nawaza kuwajibu wana Vingunguti kwanini Kumbilamoto amehama CUF" amesema Mbulu.
"Nimeachia nyadhifa zangu zote zikiwemo za Serikali na kujiunga CCM, Mimi sio mjinga nimepima kina cha Maji nikaona siwezi kuyavamia na nimeungana na Ndugu yangu Kumbilamoto kwani ameniachia majukumu mwezi sasa sitoki nje nawaza kuwajibu wana Vingunguti kwanini Kumbilamoto amehama CUF" amesema Mbulu.


0 Maoni